Old school Easter eggs.
Sm gen 2 1 thumb 30
Kuna Mume na Mke ,walienda shambani na kuukuta uyoga mzuri ila hawakuwa na uhakika kama uyoga ule haukuwa na sumu. Walikubaliana kumpa mbwa ilikujidhibitishia. Walipofika nyumbani walipika na kisha kumpa mbwa. Siku hiyo mbwa hakupata madhara yoyote. Siku iliyofuata baada ya akuamka cha kwanza ni kumtazama mbwa. Mbwa alikuwa salama salimin! Wakajiridhisha kuwa uyoga hauna sumu. Wakaenda shamba na kuchuma uyoga wa kutosha. Waliporudi mke aliuandaa na familia yote ikala. Ilipofika saa 12 jioni mtoto aliingia kasi na kusema: "Baba mbwa amekufa,anatoa damu mdomoni" hapo wakajua kuwa kumbe uyoga unaua,taratibu hivyo na wao kesho watakufa.NO WAY OUT. Wakaanza kutubu dhambi zao. Mume akaanza "Mke wangu kabla ya sijafa naomba unisamehe sana kwani nilikuwa natembea na mdogo wako na ile mimba aliyotoa ilikuwa yangu". Nisamehe mke wangu ili Mungu nae anisamehe, huku akiwa amepiga magoti Mke nae "sawa nimekusamege. Ila na we naomba unisamehe kabla sijafa. Mume "sema tu mke wangu nitakusamehe mbona we umenisamehe"........Mke "Huyu mtoto wa mwisho sio wako ni wa yule rafiki yako kipenzi(pia ni jirani yao) nisamehe mme wangu. Mme akasikitika sana..... Mara anaingia mtoto yule yule wa mwisho na kusema "Baba yule mtu aliyemgonga mbwa kwa baskeli kasema atakuja kesho muongee. Ila mbwa amepona nilikua nacheza nae sasa hivi kumbe alizimia tu..VIPI KUHUSU HII NDOA ITAENDELEA KWELI?