Mtoto mmoja mwenye umri
wa miaka 9 alikuwa anahitaji
sana sh. 100,000(laki moja),
akamuuliza mama yake ni
jinsi gani anaweza kupata
pesa hizo. Mama yake akamwambia "muombe"
Mungu atakupatia. Mtoto
alianza kuomba kila siku na
kila mara lakini hakupata
hiyo pesa toka kwa Mungu.
Hatimaye akafikia uamuzi wa kumuandikia barua Mungu ili
asome maombi yake kisha
akaipost barua ile.
Wakati wafanyakazi wa
posta wakichambua barua
kwa ajili ya kuzipeleka sehemu
husika,walishangazwa kuona
bahasha iliyoandikwa "kwa
mwenyezi Mungu" na
wakashindwa kuelewa
mahali pa kuipeleka wakaamua kuifungua, Barua
ilisomeka hivi: " Mpendwa Mungu,jina langu
ni EMMANUELEY, nina umri wa
miaka 9 na ninasoma darasa
la tatu katika jiji la Dar es
salaam ambalo liko katika
nchi ya Tanzania,Bara la Afrika. Nimeamua
kukuandikia barua hii
kukuomba kiasi cha shilingi
laki moja baada ya kuomba
bila kupata majibu toka
kwako. Naomba sana unisaidie kwani mimi ni
mtoto mdogo na sina uwezo
wa kufanya kazi na kupata
pesa. Pia wazazi wangu
hawana uwezo,kwani hata
nchi yetu ni maskini..Shukrani WAKO
MTIIFU, Emma Wafanyakazi wa posta
walifurahishwa sana na barua
hiyo na kisha wakaamua
waipeleke kwa Rais KIKWETE.
Rais Kikwete naye
alipoipokea ilimfurahisha sana,kisha akamwambia
secretary wake achukue sh.
2000 amtumie mtoto huyo
akidhani kuwa pesa hizo
ataziona kuwa nyingi sana.
Mtoto huyo alipopokea hizo sh.2000 alijibu hivi: "Mpendwa Mungu wangu,
nashukuru sana kwa
kusikiliza maombi yangu na
kunitumia pesa
nilizokuomba. Lakini
nimebaini kuwa uliamua kuzituma kupitia serikali yetu
ya Tanzania. Kama
ilivyokawaida yao hao
wezi,wamekata kiasi cha sh.
98,000,kwa ajili ya Kodi,kwa
hiyo wameniletea sh.2000 tu.